DKT. BAGHAYO SAQWARE ATOA ELIMU KUHUSU BIMA KWA MAAFISA UNUNUZI
                                
                                
                                
                                
                                
                            
                        
                                
                                     
                                    13 Dec, 2023
                                
                            
                        
                            Leo tarehe 13Desemba 2023, Kamishna wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA) Dkt. Baghayo Saqware ametoa elimu kuhusu bima kwa Maafisa ununuzi wanaoshiriki Mkutano wa 14 wa Wataalam wa Ununuzi na Ugavi unaofanyika Jijini Arusha. Kamishna kwenye Mkutano huo ameambatana na Watumishi wengine wa Mamlaka ( TIRA). Mapema jana Desemba 12, 2023 Waziri wa Fedha Mhe. Mwigulu Nchemba alitembelea banda la TIRA na kupewa maelezo juu ya shughuli za TIRA na Sekta ya bima kwa Ujumla. TIRA-kwa Soko Salama la Bima.
            