Mkutano Mkuu wa Bima Tanzania (Annual Insurance Day 2025): TIRA wapongezwa kwa maendeleo sekta ya bima nchini;

Juni 20, 2025
Mkutano huo umefunguliwa rasmi na Katibu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi, Mhandisi. Zena A. Said katika hoteli ya Gran Melia, Arusha ambapo aliipongeza TIRA kwa ufanisi katika utendaji wake na kufanikiwa kukuza sekta ya bima. Pia alipongeza maandalizi mazuri yaliyofanyika kuelekea Mkutano huo kama Bima Sport Bonanza, Matembezi ya bima (Bima Walk), Bima Debate na Urudishaji kwa jamii CSR.
Kwa upande wake Kamishna wa Bima Tanzania Dkt. Baghayo Saqware alieleza mafanikio na mikakati katika sekta hiyo na kutoa Rai kwa watoa huduma kuongeza ufanisi ili kuwafikia watanzania wengi zaidi kutumia bidhaa za bima.
Mkutano huo umehudhuriwa na watendaji wakuu wa kampuni za bima, washauri wa bima, mawakala wa bima na wadau wengine katika sekta hiyo muhimu katika kukuza uchumi wa taifa letu.
TIRA KWA SOKO SALAMA LA BIMA