Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania

TIRA Logo
TIRA Ndani ya Wiki ya Utumishi wa Umma Dodoma
17 Jun, 2025
TIRA Ndani ya Wiki ya Utumishi wa Umma Dodoma

Maonesho hayo yenye lengo la kukutanisha Taasisi mbalimbali za Umma katika kuelimisha majukumu yake kwa wananchi  yatadumu kwa wiki moja, kuanzia tarehe 16 hadi 23 Juni 2025, yakiwa na kaulimbiu isemayo “Himiza matumizi ya mifumo ya kidijiti ili kuongeza upatikanaji wa taarifa na kuchagiza uwajibikaji”. 

Katika banda la TIRA, wananchi wanapata fursa ya kujifunza kuhusu huduma mbalimbali za bima, haki na wajibu wa mteja wa bima lakini pia fursa za kiuchumi zinazopatikana katika sekta ya bima.

TIRA wapo tayari kutoa elimu ya moja kwa moja kwa wananchi kuhusu umuhimu wa bima katika maisha ya kila siku ikigusia bima zote mathalani bima ya afya, bima za gari, biashara, bima ya kilimo, bima katika uvuvi na ufugaji na bima nyingine kujikinga na majanga mbalimbali. Vilevile  wananchi wanapata elimu kuhusu teknolojia mpya katika mifumo ya TEHAMA ya TIRA  kama TIRAMIS, katika kusimamia sekta ya bima nchini.

Hii ni fursa nzuri kwa wananchi na wadau wote wa sekta ya bima kutembelea banda la TIRA, kupata huduma, kutoa maoni na kuuliza maswali.

Karibu ujifunze, uelimike!

TIRA KWA SOKO SALAMA LA BIMA