Tunarudisha kwa Jamii; Wadau Sekta ya Bima wachangia madawati Shule ya Msingi Meru Arusha

Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA) kwa kushirikiana na Taasisi ya Bima Tanzania (IIT) pamoja na wadau wengine kama Kampuni za Bima leo Juni 18, 2025 wamefanya tukio la urudishaji kwa jamii (CSR) kwa kuchangia madawati katika shule ya Msingi Meru iliyopo Halmashauri ya Jiji la Arusha, ikiwa ni tukio kuelekea Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Siku ya Bima Tanzania hapo Juni 20, 2025.
Awali, wadau hao wa bima walikutana na Mkuu wa Wilaya, Halmashauri ya Jiji hilo Bw.Joseph Mkude ambaye alishukuru kwa msaada huo wa madawati na kuahidi kuendeleza ushirikiano na sekta ya bima, pia kujumuika katika matembezi ya uhamasishaji wa matumizi ya bima (Bima Walk) hapo tarehe 19 Juni 2025.
Aidha katika tukio hilo Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo Bw. Ibrahim Ndee aliishukuru TIRA na wadau hao wa bima kwakuwa madawati hayo yatasaidia kupunguza adha ya watoto kusongamana. Pia Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Siku ya Bima Tanzania, Bw, Jared Awando aliwaasa wadau wa bima kuendeleza umoja na kurudisha kwa jamii ili kukuza sekta mbalimbali.
Pia Meneja wa TIRA Kanda ya Kaskazini Bw. Bahati Ogolla akimwakilisha Kamishna wa Bima Tanzania, ameeleza Mamlaka kama wadau wa elimu wamekuwa wakitoa msaada mbalimbali kwa jamii lakini pia kama wadau wa elimu kukuza sekta hiyo nchini.
TIRA KWA SOKO SALAMA LA BIMA