Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania

TIRA Logo
Wiki ya Utumishi wa Umma: Katibu Mkuu Utumishi Atembelea Banda la TIRA, Asisitiza Bima kwa Magari ya Serikali
18 Jun, 2025
Wiki ya Utumishi wa Umma: Katibu Mkuu Utumishi Atembelea Banda la TIRA, Asisitiza Bima kwa Magari ya Serikali

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Juma Mkomi, ametembelea banda la Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA) katika Maonyesho ya Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma 2025 yanayofanyika katika viwanja vya Chinangali Park, jijini Dodoma.

Bw. Mkomi amesisitiza umuhimu wa uchapakazi na uwajibikaji kwa watumishi wa umma ili kuongeza weledi na ufanisi katika utekelezaji wa shughuli za Serikali.

Aidha, akiwa katika banda la TIRA, ameeleza umuhimu wa magari ya Serikali kukatiwa bima ili kuhakikisha yanakuwa na kinga dhidi ya majanga, jambo litakalosaidia kuipunguzia Serikali hasara iwapo ajali au madhara yatatokea.

Kwa sasa, TIRA inaendelea kuishauri Serikali umuhimu wa kukatia bima magari yake yote kama sehemu ya usimamizi wa rasilimali na ulinzi wa mali za umma.

TIRA KWA SOKO SALAMA LA BIMA