Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania

TIRA Logo
TIRA yashiriki Maadhimisho Wiki ya Usuluhishi – elimu ya bima na usuluhishi yatolewa
17 Apr, 2026
TIRA yashiriki Maadhimisho Wiki ya Usuluhishi – elimu ya bima na usuluhishi yatolewa

TIRA yashiriki Maadhimisho Wiki ya Usuluhishi – elimu ya bima na usuluhishi wa malalamiko ya bima wafanyika

Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA) imeshiriki kikamilifu katika Wiki ya Usuluhishi wa Migogoro kuanzia tarehe 13 hadi 17 Aprili 2026, jijini Dar es Salaam, kwa lengo la kuelimisha umma kuhusu njia mbadala za utatuzi wa migogoro, hususan katika sekta ya bima.

Kupitia ushiriki huo, TIRA ilitoa elimu kwa wananchi juu ya taratibu za kushughulikia malalamiko ya bima, haki na wajibu wa wateja pamoja na umuhimu wa kutumia njia za usuluhishi  badala ya kwenda mahakamani.

Aidha, TIRA imeshiriki vikao vya usuluhishi ambavyo vimejumuisha watumiaji wa huduma za bima wenye malalamiko ya fidia pamoja na  kampuni za bima; akieleza kuhusu vikao hivyo leo Aprili 17, 2024 Meneja wa TIRA Kanda ya Mashariki amesema vimekuwa vya manufaa makubwa ambapo zaidi ya usuluhishi wa malalamiko hayo pia elimu ya bima imetolewa kwa wahusika.

Naye, Mzee Pauli Temba mmoja wa mshiriki wa vikao vya usuluhishi ameishukuru TIRA kwa elimu aliyopata pamoja na namna utatuzi wa malalamiko yake ulivyofanyika kwa kukutanisha pande zote.

Wiki ya Usuluhishi imeratibiwa na Kituo cha Usuluhishi kutoka Mahakama kuu ya Tanzania ambapo pia Ofisi ya Msuluhishi wa Migogoro ya Bima (TIO), Kampuni za bima za Heritage, CRDB, Sanlam Allianz zimedhamini maadhimisho hayo.

TIRA KWA SOKO SALAMA LA BIMA