Bima Sports ilivyokonga nyoyo: Wadau sekta ya bima waonesha uwezo katika kabumbu na michezo mingine

Mei 31, 2025 ilikuwa siku njema sana kwa wapenzi wa michezo hasa wadau sekta ya bima, Bima Sports ilipamba moto katika viwanja vya Tanzanite Sports Hub Mikocheni. Katika tukio la kusisimua zaidi Kamishna wa Bima Tanzania Dkt. Baghayo Saqware alichezesha mechi iliyowakutanisha wakuu wa kampuni za bima.
Michezo ni afya, Bima Sports ni kionjo kingine katika shamrashamra za kuelekea Siku ya kilele cha Bima Tanzania ambapo kwa mwaka huu wa 2025 tukio hilo litafanyika June 18 – 21 jijini Arusha. Bima Sports ilikuwa na michezo mbalimbali ukiwemo mchezo wa mpira wa miguu, riadha na mchezo wa kukimbiza kuku.
Timu ya mpira wa miguu kutoka Mamlaka ilishiriki na kufanya vizuri lakini bahati ya mtende kwa mwaka huu iliwaangukia kampuni ya Bima ya CRDB ambao walitwaa kombe. Aidha, ushindi mwingine ulienda kwa raisi wa taasisi ya bima (IIT) Bi. Margaret Ikongo aliyeibuka kidedea katika mchezo wa kukimbiza kuku.
Endelea kufatilia kuhusu yatakayojiri Siku ya Bima Tanzania hivi karibuni.
#Michezoniafya
#TanzaniaInsuranceDay2025
#TIRA KWA SOKO SALAMA LA BIMA