Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania

TIRA Logo
Elimu ya bima yatolewa kwa wanawake wajasiriamali Arusha
23 Mar, 2026
Elimu ya bima yatolewa kwa wanawake wajasiriamali Arusha

Kuelekea kilele cha Mkutano wa Wanawake katika Sekta ya Fedha unaoratibiwa na TAWiFA hapo kesho, leo Machi 22, 2026; TIRA na TIO wametoa elimu ya bima kwa wanawake wafanyabiashara wa Mkoa wa Arusha katika ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa huo. 

Akizungumza katika Mkutano huo Msuluhishi wa Migogoro ya Bima Bi. Margaret Mngumi ametoa rai kwa wanawake kukatia bima biashara zao ili waweze kulipwa pale ambapo janga litatokea na kusisitiza endapo kutakuwa na changamoto yoyote katika ufatiliaji wa madai ya bima baada ya majanga Ofisi husika ambayo ni Ofisi ya Msuluhishi wa Migogoro ya Bima Tanzania (TIO) itashughulika moja kwa moja katika utatuzi wa changamoto hizo kwa njia ya usuluhishi ya haraka

Aidha, elimu ya Matumizi ya Mifumo rasmi ya Kifedha imetolewa ambapo wanawake wameaswa kuitumia ili kutunza pesa zao kwa matumizi mbalimbali yakiwemo kukata bima za maisha, bima za biashara, bima za afya, bima za elimu kwa ajili yao na familia zao kwa jumla.

Kamishna wa Bima na Naibu Kamishna wa Bima wanatarajiwa kuhudhuria Mkutano huo wenye lengo la kuongeza ujumuishi wa wanawake katika masuala ya kifedha na utoaji elimu ambao utafanyika PAPU Tower, jijini hapo.

TIRA KWA SOKO SALAMA LA BIM