Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania

TIRA Logo
Tunashiriki Tanzania Dental Expo: Karibu ufahamu wajibu wetu kwa watoa huduma za afya
31 May, 2025
Tunashiriki Tanzania Dental Expo: Karibu ufahamu wajibu wetu kwa watoa huduma za afya

Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania kupitia Kanda ya Mashariki  inashiriki   maonesho ya siku mbili ya ‘Tanzania Dental Expo” ambayo yamekusanya watoa huduma za kinywa na wadau wengine wa afya, yanayofanyika mlimani city, Dar es salaam na yameanza Mei 30 – 31 2025.

Aidha, katika maonesho hayo TIRA inatoa elimu ya bima  kwa washiriki lakini pia kuwasisitiza watoa huduma za afya kufanya usajili kupitia mfumo wa ORS.  TIRA ina jukumu la kusajili vituo vya afya vinavyotoa huduma kupitia bima za afya.

Maonesho haya  ni muendelezo wa utoaji elimu ya bima kwa umma ili kuweza kufikia malengo ya Mamlaka na ya Serikali kwa ujumla kuongeza uelewa na matumizi ya bima nchini. 

TIRA KWA SOKO SALAMA LA BIMA